Methali na semi za Kibajuni (1)

Proverbs and sayings of the Bajuni community.

  1. Usivone dhombo kupicha na ungama ulimui.
  2. Wako kimpa mai wa ndruo muenge sana.
  3. Rafiki hukusaidia kwa kula hufawa na ndhawa nawe ikupachapo ghafula.
  4. Damu si mai.
  5. Usibike dhumbe ungama huyaiva ulipo.
  6. Ajali haina kinga
  7. Chendra wema wendre dhako
  8. Mwenye pupa hadiriki kula ṯamu
  9. Alimao mmoya walai ni vangi
  10. Ukivunḏa ada utadhaa kwa shida.
  11. Ṯamu iko kachika uṯungu.
  12. Rivu haipachi nke.
  13. Jirani ni aula.
  14. Shaba kushindra dhahabu elewa ni kidunia
  15. Kuna nadhi nnadhini wala makumbi haina
  16. Akufukudhae hakwambii ṯoka
  17. Akufaae kwa dhiki ndrie rafiki
  18. Kilio hulia mweṉe na nchu mbali kalia
  19. Shirika halina wema na nla pweke hakuna
  20. Kama halifuliwi mayi na mataruma hudhama