Methali na Semi za Kibajuni (3)

Proverbs and sayings from the Bajuni community.

  1. Upecheo ndriwe
  2. Ṉumba ikosao nshindo mwana hanyamai
  3. Usiku nmwangala ntumbuu huva papa
  4. Ṯaṯedhae na Mwarabu na iguu lenyu imoya.
  5. Kuketi si kama kwendra
  6. Nvundaṯi ni mwanaṯi
  7. Akukachae nsipa nawe nvunde mfupa
  8. Sinbike shoe dhicha ndrie mboni wa dhia
  9. Nchu ni ndrue na damu haifuchiki
  10. Samaki mpija mashudhi hakangwi kwa mafucha ya ucho
  11. Ni mocho hakubisiki dhidi mbuyu uye Pwani
  12. Ndhinga dhinga hukucha na mwendati hukuvaa
  13. Dhifudhao ni dha Rwabi, endhi dha nja hukoma
  14. Mai a pwani huvava na atavava daima
  15. Iganda la muwa la yana ṯungu mefanya ni pacho
  16. Mgagaa na upwa hali wali nkavu
  17. Usiaṯe mbachao kwa nswala upichao
  18. Ishe kunvaka inya valivadhaa vana
  19. Nchi nviṯi sipandre na nkavu sirevereve
  20. Avavie kisimani na nṯungini si ṯamu