Methali na Semi za Kibajuni (4)

Proverbs and sayings of the Bajuni community.

  1. Ulie wali bario uchekechee nkono
  2. Aso kuveko na lake haliko
  3. Umasikini si ila nchu ndrue hanṯeki
  4. Mungasumbuka vaja alie mbee u mbee
  5. Nchu nkukuche mwengeni maṯo
  6. Ukipawa kula ila kwa kuiva na ipawa lina miva
  7. Alivachao mai hali nchupu
  8. Nchu ndrue hanyavi ni akiba a kesho
  9. Ukenda nyi wa ṯongo lako iṯo funga.
  10. Ṯungu angamea mbava makadhi ake ni iṯi
  11. Twahara ya ijumaa hufanywa hamisi
  12. Nchu nkwavo japo ṯini mwa irara.
  13. Vachu vote vanganyuka isi huiyaliani?
  14. Nchu ndruwe haṯa kama udhidhie
  15. Ichumbo liloshiba halichambui alodhaa
  16. Ukimvona kobe menyamisa kiṯwa uive hupanga sheria
  17. Bahari ikichafuka madhimbi henda nsako
  18. Gonga igogo ulisikie nlio
  19. Dha kale hadhinuki
  20. Nla nawe hafi nawe ile ndhaliwa nawe